Mgomo wa mawakili wakwama
Ule mgomo ulioitishwa na baraza la uongozi wa chama cha mawakili Tanganyika TLS umeshindwa kufanyika kutokana na mawakili hao kuhudhuria vik...

Ule mgomo ulioitishwa na baraza la uongozi wa chama cha mawakili Tanganyika TLS umeshindwa kufanyika kutokana na mawakili hao kuhudhuria vikao vya Mahakama na mabaraza mbalimbali kama ilivyo kawaida ya siku zoto.
Mwandishi wa habari hizi amefika katika mahakama mbalimbali na kushuhudia idadi kubwa ya mawakili wakihudumu kama kawaida juhudi za kiuandishi kuwapata viongozi wa chama hicho ili wazungu,zie mgomo wao hazikuzaa matunda.
Hata hivyo miongoni mwa mawakili walioonekana katika Mahakama kuu ni Profesa Safari juhudi za kuongea nae hazikuzaa matunda, hata hivyo mwandishi alibahatika kuongea na Wakili mmoja bw Masawe wakili wa siku nyingi ambae alionyesha kutfurahishwa na namna uongozi wa chama chao unavyoendeshwa mamb
Sifurahishwi kabisa na namna viongozi wa chama chetu wanavyotuongoza angalia hata hili suala la mgomo limefanywa kwa pupa ndio maana hatukuona sababu ya kulitii alisema bw Masawe.